Ni Ugonjwa wa mahindi unaosababishwa na virusi. Ugonjwa huu husababishwa na muunganiko wa virusi vya aina mbili: Virusi vya Mabaka na Madoa ya Mahindi-Maize Chlorotic Mottle Virus (MCMV) na mojawapo kati ya virusi vifuatavyo: Virusi vya Batobato ya Miwa-Sugarcane Mosaic Virus (SCMV), Virusi Vidumaza vya Batobato ya Mahindi-Maize Dwarf Mosaic Virus (MDMV) na Virusi Michirizi vya Batobato ya Ngano-Wheat Streak Mosaic Virus (WSMV)